BANDARI YA DAR ES SALAAM- BANDARI KUU UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI NA KATI

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi sita wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki  utakaojadili masuala ya usafirishaji ...

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi sita wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki  utakaojadili masuala ya usafirishaji na uchukuzi.
Waziri wa Uchukuzi nchini SAMUEL SITTA amewaambia waandishi wa habari jijini DAR ES SALAAM kuwa katika mkutano huo utakaofanyika machi 26, marais sita kutoka nchi hizo watazindua safari za treni ya mizigo kutoka Tanzania kupitia Rwanda  ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo.
Waziri wa uchukuzi Samwel Sitta akizungumza na viongozi wa
DRC kongo na waandishi wa habari jijini dsm leo
PICHA:NA LIVINGSTONE MINJA

Aidha waziri SITTA ameongeza kuwa katika mkutano huo marais kutoka nchi za KENYA,BURUNDI,RWANDA,UGANDA,NA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO wakiongozwa na rais JAKAYA KIKWETE wataafikiana masuala mbali mbali ya ushirikiano katika sekta ya usafirishaji ikiwemo matumizi ya bandari ya Dar es salaam kama bandari kuu kwa ukanda wa afrika mashariki na kati.
waandishi na washiriki mbalimbali wakufuatilia mkutano huo wa
  Mh. Sitta na viongozi wa Kongo
PICHA:NA LIVINGSTONE MINJA
 Sitta ameongeza kuwa katika mkutano huo marais kutoka nchi wanachama wa afrika mashariki na kati watazindua safari za treni ya mizigo kutoka TANZANIA kupitia RWANDA mpaka JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO katika kurahisisha usafirishaji wa mizigo baina ya nchi hizo.
waziri wa uchukuzi wa nchini drc Kongo
Mh. Justin Kalumba Mwana ngongo
PICHA:NA LIVINGSTONE MINJA




Kwa upande wake waziri wa uchukuzi  kutoka  jamhuri ya kidemokrasia ya kongo Bw.JUSTINE KALUMBA MWANA NGONGO ameipongeza serikali ya Tanzania kwa jitihada zake katika sekta ya usafirishaji  na kumshukuru rais JAKAYA KIKWETE kwa kukubali TANZANIA kuwa wenyeji wa mkutano huo.

Related

Habari 37419106576610979

Post a Comment

emo-but-icon

Recent Post

Comments

Hot in week

My Blog List

Recent

item