HILI NDILO DUKUDUKU LA WAFANYABIASHARA JUU YA MASHINE ZA EFD KWA WAZIRI KIGODA
wafanyabiashara jijijni dar es salaam leo wamefanya mkutano wa aina yake wakiwa Waziri wa viwanda na biashara Mh. Abdallah Kigoda ikiwa n...
https://mzukatz.blogspot.com/2014/01/hili-ndilo-dukuduku-la-wafanyabiashara.html
wafanyabiashara jijijni dar es salaam leo wamefanya mkutano wa aina yake wakiwaWaziri wa viwanda na biashara Mh. Abdallah Kigoda ikiwa na lengo la kutoa madukuduku yao mbalilmbali ambayo yameonekana kuwa sugu na kikwazo kikubwa katika ufanyaji wao wabiashara.
mkutano huo ulioshamiri hisia huku wafanyabiashara hao kuonekana wakiongea kwa ghadhabu kubwa pia ulihusisha wawakilishi mbalimbali ikiwemo upande wa wasanii wa bongo muvie uliowakilishwa na Steve Nyerere.
kikubwa katika mkutano huo iliikuwa ni kuhusiana na mashine za EFD zinazohusika na utoaji wa risiti pamoja na makato ya kodi. wafanyabiashara hao wamesema mashine hizo ni mpango wa serikali kuwanyonya na kuwarudisha nyuma na kuwa hazina faida yoyoyte kwa wafanyabiashara hao ikianzia kwa wafanyabiashara wa chini, kati na wakubwa.
pia mkutano huo ulihusisha wawakilishi kutoka jeshi la polisi ambapo wamewakilishwa na kamishna msaidizi bw. Lazaro Mambosasa pamoja na wawakilishi kutoka mikoa mingine ikiwemo tabora, singida na zanzibar
Pia
kwa upande wake Waziri Kigoda ametoa ahadi kwa wafanyabiashara hao kuwa malalamiko yao ameyasikia na ataanza kutekeleza urekebishwaji wake mara moja.
waziri wa biashara na viwanda Mh. abdallah Kigoda akiongea na wafanyabiashara katika mkutano uliofanyika diamond jubilee. |
wafanyabiashara wakiwa wamesisimama kama ishara ya kumbukumbu ya heshima kwa aliyekuwa waziri wa fedha marehemu Willliam Mgimwa. |
wafanyabiashara wakifuatilia kwa ukaribu mkutano wa wafanyabiashara katika ukumbi wa diamondi jubilee |