Angalia Uzinduzi kampeni wa Chama Cha Mapinduzi CCM jijini DSM- full video

 Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amefungua pazia la kampeni za chama hicho kwenye Viwanja vya Jangwani katika tukio lililohudhuri...

 Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amefungua pazia la kampeni za chama hicho kwenye Viwanja vya Jangwani katika tukio lililohudhuriwa na maelfu ya wananchi, huku akieleza mambo 25 atakayoyafanya iwapo Watanzania watamchagua kuwa Rais wa Awamu ya Tano.

Huku akitumia maneno: “Mimi kazi tu”, “Tanzania ya Magufuli ni ya viwanda”, Dk Magufuli aliyetumia dakika 53 kueleza sera zake, kuanzia saa 11.40 hadi 12.33 jioni alisema Watanzania wanataka kitabu kipya cha mabadiliko na yeye na mgombea mwenza, Samia Suluhu ndiyo wanaoweza kuyaletea.
Dk Magufuli ambaye ni Waziri wa Ujenzi, alizungumza lugha za makabila saba kama ishara ya kuonyesha mshikamano wa Watanzania, huku makundi mbalimbali kama madereva, mama lishe na mengine yaliyokuwapo uwanjani hapo yakipaza sauti kutaka kusikia atawasaidia vipi akiingia Ikulu, ombi ambalo mgombea huyo aliwajibu na kutuliza kiu yao.
Mgombea huyo wa urais wa CCM aliahidi kuanzisha mahakama maalumu ya kusikiliza kesi za rushwa na ufisadi, kumaliza tatizo la wanafunzi wa elimu ya juu kukosa mikopo, kuhakikisha mama lishe hawabughudhiwi, kusimamia haki za wasanii, kulinda Muungano na usalama wa nchi.

Related

Video 657093775205791949

Post a Comment

emo-but-icon

Recent Post

Comments

Hot in week

My Blog List

Recent

item