Kuelekea siku ya kifua kikuu duniani... Wizara ya Afya yasema haya...

Watanzania wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kupima afya zao katika vituo mbalimbali vya afya nchini katika maadhimisho ya siku ya kifua ki...

Watanzania wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kupima afya zao katika vituo mbalimbali vya afya nchini katika maadhimisho ya siku ya kifua kikuu duniani yanayotarajiwa kufanyika kesho tarehe 24/03/2015 duniani kote ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘’IBUA,TIBU,PONYA KILA MGONJWA WA TB’’
Katibu mkuu wizara ya afya na ustawi wa jamii Bw DONALD MMBANDOPICHA:LIVINGSTONE MINJA
Hayo yamesemwa na katibu mkuu,wizara ya afya na ustawi wa jamii Bw.DONALD MMBANDO wakati akitoa taarifa juu ya maadhimisho hayo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa maadhimisho hayo yana lengo la kuamsha ari kwa wadau mbalimbali wa afya nchi kuunganisha  nguvu zao katika mapambano juu ya ugonjwa wa kifua kikuu.

Hata hivyo Bw.DONALD amesema kuwa amesema kuwa kifua kikuu ni miongoni mwa magonjwa angamizi hapa nchini na kusema kuwa wadau wa afya nchini  wanaongeza uchunguzi wa kutambua wagonjwa zaidi wa kifua kikuu nchini .

Aidha ameongeza kuwa kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza na unasababishwa na vimelea aina ya bacteria wanaojulikana kama mycobakteria huku akisema kuwa utafiti unaonyesha kuwa zaidi ya  asilimia 30 ya vifo vya walioathirika na ugonjwa wa ukimwi vinatokana na kifua kuu.

meneja mpango wa taifa wa kuthibiti kifua kikuu nchini Dk BEATRICE MUTAJOBA
PICHA:LIVINGSTONE MINJA
Kwa upande wake meneja mpango wa taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma nchini Dokta BEATRICE MUTAJOBA amesema kuwa matokeo ya tiba ya kifua kuku nchini ni mazuri kwa wagonjwa wengi ambapo zaidi ya asilimia 40 ya wagonjwa wamepona kabisa ugonjwa huo huku akiwataka watanzania wenye dalili za ugonjwa wa kifua kikuu kujitokeza na kuwahi kupata huduma kwa haraka zaidi.


_imeandikwa na Praygod Thadey

Related

Habari 685059716813777877

Post a Comment

emo-but-icon

Recent Post

Comments

Hot in week

My Blog List

Recent

item